advanced Search
KAGUA
22374
Tarehe ya kuingizwa: 2012/03/10
Summary Maswali
je mwenye saumu anaruhusiwa kukoga janaba?
SWALI
je inafaa mtu kukoga janaba hali akiwa amefunga?
MUKHTASARI WA JAWABU

Mtu anaweza kupatwa na janaba katika hali mbili: ima itakuwa ni kabla ya adhana ya asubuhi au baada ya adhana ya asubuhi, lakini janaba tunalolizungumzia hapo ni lile janaba la dharura, kama vile dharura ya kuota, siyo la kupiga ponyeto au kujamii.

Kukoga janaba kabla ya dhana ya asubuhi:

Kauli ya imam khomeiniy inasema: iwapo mtu atabakia na janaba kwa makusudi hadi wakati wa adhana ya asubuhi ukaingia, au iwapo yeye alikuwa anawajibika kutayamamu lakini akawa hakutayamamu, na akawa amefanya hivyo kwa makusudi, funga yake itabatilika.[1]  Lakini iwapo yeye atakuwemo ndani ya funga nyengine ya wajibu maalumu, kama kama vile funga ya nadhiri, funga yake itakuwa ni sahihi.[2]

Kwa hiyo iwapo mtu atakutwa na janaba ndani ya saumu ya Ramadhani, na tokeo hilo likawa ni kabla ya adhana ya asubuhi, mtu huyo atatakiwa kukoga janaba.

Kukoga janaba baada ya adhana ya asubuhi na kuendelea kipindi kizima cha mchana:

Kauli ya imam Khomeiniy: iwapo mwenye funga ataingiwa na janaba ndani ya mchana (hali akiwa amelala), hakutokuwa na ulazima kukoga papo hapo[3], lakini atawajibika kukoga janaba pale atapotaka kusali adhuhuri, alasiri, magharibi au ishaa. Na wakati wowote ule mtu atakapoamka baada ya adhana ya asubuhi ndani ya mwezi wa Ramadhani, na akajikutia kuwa ana janaba, hata kama atakuwa anajuwa kuwa janaba hilo limempata kabla ya adhana hiyo, funga yake itakuwa ni sahihi.[4]

Kwa hiyo wakati wowote ule mtu akiwemo ndani ya saumu anaweza kukoga janaba.

 


[1] Taudhihul-masaail chenye sherehe ya imam Khomeiniy, juz/1, uk/908-909, suala la 1619. Kauli ya Makaarim Shirazi ni kwamba: ni wajibu kuchukuwa tahadhari ya kuihesabu funga yake kuwa ni batili, lakini iwapo atakuwa hana uwezo wa kukoga au akawa na dhiki ya wakati, anatakiwa kutayamamu, lakini iwapo atakuwa yeye hakufanya hivyo kwa makusudi, basi funga yake itakuwa ni sahihi. Kauli ya Faadhil Lankaraniy: mtu anayetaka kufunga Ramadhani au kulipa funga za Ramadhani, hatakiwi kubakia na janaba kwa makusudi hadi wakati wa adhana ya asubuhi, hivyo basi iwapo yeye atakuwa hakukoga na pia kwa kutokana na dhiki ya wakati akawa hakutamamu, funga yake itabatilika. Kukaa na janaba katika funga nyengine, iwe ni kwa makusudi au si kwa makusudi, huwa hakuleti madhara juu ya funga hizo. Kauli ya Safi Gulpeigaaniy: iwapo mtu atabakia na janaba ndani ya Ramadhani hadi adhana  ya asubuhi bila  ya kukoga, pia akawa hakutayamamu, lakini akawa hakuwa na makusudio ya kufanya hivyo, bali labda  kulikuwa kuna mtu aliyemzuia kufanya hivyo, funga yake itakuwa ni sahihi.

[2] Rejea kitabu kilichopita, uk/909, suala la 1620. Kauli ya Khui na Tabriziy: iwapo yeye atakuwemo ndani ya saumu isiyokuwa ya Ramadhani au katika kuilipa funga ya Ramadhani, bali akawa katika saumu nyengine yenye kumuwajibikia yeye katika siku maalumu, kama vile funga ya nadhiri, funga yake inaonekana kuwa ni sahihi.

[3] Rejea kitabu kilichopita, uk/915, suala la 1632. Kauli ya Faadhil Lnkaraniy: ingawaje inapendekezwa mtu kuchukuwa tahadhari ya kukoga papo hapo. Kauli ya Makarim Shirazi: ni vizuri wakati wowote ule mwenye saumu anapopatwa na janaba kukoga papo hapo, lakini iwapo yeye  atakuwa hakukoga papo kwa hapo, funga yake haitobatilika.

[4] Rejea kitabu kilichopita, suala la1633. Kauli ya Makarim Shirazi: funga yake ni sahihi, iwe anajuwa kuwa amepatwa na janaba kabla au baada ya adhana, au awe na shaka juu ya hilo.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • ni kwa nini maombolezo ya Imamu Husein (a.s), yakapewa jina la Raudha?
    11466 تاريخ کلام 2012/05/23
    Neno (Raudha) ni neno maalumu linalotumiwa na waombolezaji wa mwauwaji ya Imamu Husein (a.s), na neno hili linatoka kwenye kitabu maarufu cha maombolezo ya Imamu Husein (a.s), kijulikanacho kwa jina la (Raudhatush-Shuhadaa), na kitabu hichi ni moja kati ya vitabu vya mwanzo vilivyonukuu tokeo la Karbala, na ...
  • nini maana ya ucha Mungu?
    21455 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Taqwa (ucha Mungu) ni nguvu maalumu za kiroho zinazo weza kupatikana ndani ya nafsi ya mwanaadamu, nguvu ambazo huwa ni himaya maalumu inayomuwezesha yeye kujitenga na maasi. Taqwa kamili ni ile inayomfanya mtu kujiepusha na maasi yanayo eleweka na kila mmoja wetu, pamoja na kujiepusha na yale ...
  • ni namna gani Qur-ani imelielezea fungamno juu ya imani na kupatikana kwa utulivvu wa moyo?
    12533 Tafsiri 2012/06/17
    Kilugha panapotumika neno Imani au itikadi, humaanisha kule mtu kukubali na kusadiki, na maana hii huwa ni kinyume cha neno kukadhibisha na kukanusha. Kitaalamu neno imani huwa linamaanisha kule mtu kusadiki na kuamini jambo fulani kimatamshi, kimoyo pamoja na kimatendo, lakini neno utulivu ambalo ni tafsiri ya ...
  • je majina ya watu watano watukufu yametajwa ndani ya Taurati na Injili?
    12829 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Kwa mujibu wa nukuu za baadhi ya Hadithi ni kwamba, majina ya matano ya Aali Abaa (a.s), yaani Aali wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambao ni: Ali, Fatima,Hasan na Husein, yametajwa ndani ya Taurati na Injili. Pia suala hilo linaonekana kuashiriwa ndani ya ile Hadithi yenye kunukuu majadilianao ...
  • je nini wajibu wa mwanamke anayenyonyesha kwa muda wa miaka miwili mfululizo? Hivi yeye atatakiwa kulipa fidia ya funga zake pamoja na kuzilipia fidia kwa kutokana na kuchelewesha kuzilipa funga hizo?
    11663 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Jawabu kutoka ofisi ya Ayatullahil-Udhmaa Sistani (Mola amlinde): 1-mwanamke ambaye ananyonyesha, aliye na uchache wa maziwa, awe ni mama wa mtoto au mlezi anayelipwa kwa ajili ya kumnyonyesha mtoto huyo, au hata kama atakuwa anamnyonyesha bure, iwapo funga itakuwa ni yenye kumletea madhara au kumletea ...
  • Shin aure yana da wasu sharaDai na musamman?.
    7053 Sheria na hukumu 2017/05/22
    A mahangar musulunci auren da’imi da na mutu’a suna da sharaDai waDanda sune kamar haka:- 1. Karanto siga (Yarjewa juna tsakanin miji da mata shi kaDai bai wadatar ba lalle ne a hada shi da furta “farar da” lafazi na musamman). 2. Bisa ihtiyaDi na wajibi ya ...
  • nini maana ya itikafu
    20533 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • nini siri hasa ya Uslamu kuwa ni dini ya mwisho, na nini pingamizi hasa ya bwana Surush juu ya hilo?
    14621 Elimu ya zamani ya Akida 2014/02/12
    Kuzingatia nukta zifuatazo kutaweza kumsaidia msomaji kulitambua vyema suala hili: 1- Hitimisho la utume lina maana ya hitimisho la dini; na hii inamaanisha kuwa hakutokuja mtume mwengine baada Yake (s.a.w.w). Hayo pia utayakuta kwenye Aya ya 40 ya Suratul-Ahzab. 2- Dini ya Kiislamu imeitwa dini ya mwisho ...
  • maisha ya kiucha-Mungu ni maisha ya aina gani? Je misngi ya maisha hayo haipingani na misingi mikuu ya maisha yetu?
    13570 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Iwapo sisi tutailelekea Qur-ani Tukufu, kisha tukaiuliza Qur-ani swali lifualato: je sisi tumeumbwa kwa ajili gani? Hapa tutaiona Qur-ani ikitujibu kwa kauli ifuatayo: " وَ ما خَلَقْتُ الْجِنَّ وَ الْإِنْسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ. " Maana yake ni kwamba: (Mimi (Mola) sikumuumba mwanaadamu wa jini, ila ...
  • Timsahın saxlanılması və digər ölkələrə satışına icazə varmı?
    8290 Sheria na hukumu 2014/05/22
    Təqlid olunan müctehidlərin cavabları bunlardır: Həzrət ayətullah Xamnei (Allah qorusun) Əti haram olan heyvanların saxlanılması və onun hətta, bu heyvanların ətlərinin yeyilməsini halal bilənlərə də satılması düzgün deyildir. Amma, aqillər nəzərində halal mənfəətə görə olsa məsələn, ətinin başqa ət yeyən heyvanlar üçün istifadəsi yaxud, dərisinin dəri sənətində ...

YALIYOSOMWA ZAIDI