advanced Search
KAGUA
8515
Tarehe ya kuingizwa: 2012/05/21
Summary Maswali
kwa nini tuwe wakalidi (wafuasi)?
SWALI
kwa nini tuwe wakalidi (wafuasi)?
MUKHTASARI WA JAWABU

Ruhusa ya kumfuata ulamaa maalumu katika matendo ya ibada za kila siku, inatakiwa kutolewa na akili ya mtu mwenyewe. Na wala ruhusa hiyo haingojewi kutoka kwa Maulamaa, huku kila mmoja akielewa umuhimu wa suala hili ndani ya maisha yake ya kila siku.

Katika hali yakawaida, mtu huwa ana sababu mbili zinanomfanya yeye kuwa ni mfuasi wa mtu maalumu:

1: Mwenendo wa kila mwenye akili huwa ni kuyatenda matendo yake kwa kupitia uoni wa kielimu aliokuwa nao, na pale anapohisi kuwa elimu yake ni changa kuhusiana na tendo analolitaka kulitenda, huwa anamuelekea mwerevu anayeutambua uhakika wa tendo hilo. Na mfano hilo ni kama vile mgonja kuenda kwa mtibabu ili amfafanulie ukweli wa magonjwa yake pamoja na kumpatia tiba ya magonjwa alionayo. Na hilo ndilo linalomfanya kila mwenye akili kumfuata ulamaa maalumu ili kupata ufafanuzi wa matendo na wadhifa wa kidini unaomuwajibikia yeye kisheria.

 

2: Kila muislamu anafahamu tosha kuwa dini yake ina maamrisho na makatazo maalmu yanayotakiwa kuzingatiwa na kila mfuasi wa dini hiyo, na ufahamu huu huwa ni dalili tosha itakayomfanya yeye kujihisi kuwa anawajibika kuyenda matendo yake kwa mujibu wa makatazo na maamrisho hayo yalivyo. Hapo ndipo anapojikuta kuwa; hana budi kufuata moja kati ya njia zifuatazo:

A: Awe na elimu ya kutosha itakayomuezesha kuyatambua maamrisho na makatazo hayo.

B: Awe na tahadhari katika matendo yake yote bila ya kufanya kosa katika uchaguzi wa matendo yake, yaani aliache kila lenye shaka na alishike kila lenye uhakika au kudhaniwa kuwa ni la sawa.

C: Awe ni mfuasi wa mwanachuoni maalumu, na matendo yake yawe yanaiegemea elimu  na mitazamo ya mwanachuoni huyo katika matendo yake yote ndani ya maisha yake ya kila siku.

 

Mtu ataposhikamana na moja kati ya njia hizi tulizozitaja, atajihisi kuwa ameyatekeleza matakwa ya dini  pamoja na wajibu wake ipaswavyo. Lakini njia ya mwazo huwa inahitajia muda mrefu ili yeye abobee kielimu, na kabla ya kuifikia daraja hiyo bila shaka atakuwa ni muhitaji wa moja kati ya njia mbili zilizobakia. Na njia ya pili nayo inahitajia mtu kuzielewa aina za haramu na halali pamoja na kuwa na elimu ya kutosha kuhusiana na hoja tofauti za wanazuoni mbali mbali kutokana na nyadhifa zinazomkabili, na hilo si jambo jepesi liwezalo kupatikana kirahisi au kufikiwa na kila mmoja. Njia pekee iliobakia ni njia ya tatu. Kwa ufafanuzi zaidi tunatakiwa kuelewa kwamba; dalili namba mbili iliopita hapo juu, inaonesha ulazima wa kumfuata mwanachoni katika masuala yote yanayodhaniwa kuwa ni wajibu au haramu pamoja na yale yanayodhaniwa kuwa ni sunna iwapo mtu atapendelea kuzitenda sunna hizo, lakini dalili namba moja inalithibitisha na kulizingatia suala la ufuasi katika aina zote za matendo. La muhimu kufahamu hapa ni kwamba suala la mtu kuweza kubakia kuwa ni mfuasi wa ulamaa wake baada ya kufa kwa mwanachuoni huyo, huwa linahitajia fatwa ya ulamaa huyo kuhusiana na suala hilo ndani ya uhai wake, iwapo yeye atakuwa hakutoa fatwa au haruhusu mtu kumfuata ulamaa wake baada ya kufariki kwake, hapo basi itambidi mtu mwenyewe ambaye ni mfuasi, kuwa na uangalifu juu ya suala hilo katika kuepukana nalo au kubakia kuwa ni mfuasi wa ulamaa wake.

Bado kuna dalili nyengine zinazohisiana na masuala ya ufuasi, lakini jukumu la kuzisimamisha dalili hizo litabakia mikononi mwa maulamaa, kwani wao ndio wajuzi zaidi wanaoutambua vyema uwanja huu.

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • ni kwa nini maombolezo ya Imamu Husein (a.s), yakapewa jina la Raudha?
    11466 تاريخ کلام 2012/05/23
    Neno (Raudha) ni neno maalumu linalotumiwa na waombolezaji wa mwauwaji ya Imamu Husein (a.s), na neno hili linatoka kwenye kitabu maarufu cha maombolezo ya Imamu Husein (a.s), kijulikanacho kwa jina la (Raudhatush-Shuhadaa), na kitabu hichi ni moja kati ya vitabu vya mwanzo vilivyonukuu tokeo la Karbala, na ...
  • nini maana ya ucha Mungu?
    21455 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Taqwa (ucha Mungu) ni nguvu maalumu za kiroho zinazo weza kupatikana ndani ya nafsi ya mwanaadamu, nguvu ambazo huwa ni himaya maalumu inayomuwezesha yeye kujitenga na maasi. Taqwa kamili ni ile inayomfanya mtu kujiepusha na maasi yanayo eleweka na kila mmoja wetu, pamoja na kujiepusha na yale ...
  • ni namna gani Qur-ani imelielezea fungamno juu ya imani na kupatikana kwa utulivvu wa moyo?
    12533 Tafsiri 2012/06/17
    Kilugha panapotumika neno Imani au itikadi, humaanisha kule mtu kukubali na kusadiki, na maana hii huwa ni kinyume cha neno kukadhibisha na kukanusha. Kitaalamu neno imani huwa linamaanisha kule mtu kusadiki na kuamini jambo fulani kimatamshi, kimoyo pamoja na kimatendo, lakini neno utulivu ambalo ni tafsiri ya ...
  • je majina ya watu watano watukufu yametajwa ndani ya Taurati na Injili?
    12829 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Kwa mujibu wa nukuu za baadhi ya Hadithi ni kwamba, majina ya matano ya Aali Abaa (a.s), yaani Aali wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambao ni: Ali, Fatima,Hasan na Husein, yametajwa ndani ya Taurati na Injili. Pia suala hilo linaonekana kuashiriwa ndani ya ile Hadithi yenye kunukuu majadilianao ...
  • je nini wajibu wa mwanamke anayenyonyesha kwa muda wa miaka miwili mfululizo? Hivi yeye atatakiwa kulipa fidia ya funga zake pamoja na kuzilipia fidia kwa kutokana na kuchelewesha kuzilipa funga hizo?
    11663 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Jawabu kutoka ofisi ya Ayatullahil-Udhmaa Sistani (Mola amlinde): 1-mwanamke ambaye ananyonyesha, aliye na uchache wa maziwa, awe ni mama wa mtoto au mlezi anayelipwa kwa ajili ya kumnyonyesha mtoto huyo, au hata kama atakuwa anamnyonyesha bure, iwapo funga itakuwa ni yenye kumletea madhara au kumletea ...
  • Shin aure yana da wasu sharaDai na musamman?.
    7053 Sheria na hukumu 2017/05/22
    A mahangar musulunci auren da’imi da na mutu’a suna da sharaDai waDanda sune kamar haka:- 1. Karanto siga (Yarjewa juna tsakanin miji da mata shi kaDai bai wadatar ba lalle ne a hada shi da furta “farar da” lafazi na musamman). 2. Bisa ihtiyaDi na wajibi ya ...
  • nini maana ya itikafu
    20533 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • nini siri hasa ya Uslamu kuwa ni dini ya mwisho, na nini pingamizi hasa ya bwana Surush juu ya hilo?
    14621 Elimu ya zamani ya Akida 2014/02/12
    Kuzingatia nukta zifuatazo kutaweza kumsaidia msomaji kulitambua vyema suala hili: 1- Hitimisho la utume lina maana ya hitimisho la dini; na hii inamaanisha kuwa hakutokuja mtume mwengine baada Yake (s.a.w.w). Hayo pia utayakuta kwenye Aya ya 40 ya Suratul-Ahzab. 2- Dini ya Kiislamu imeitwa dini ya mwisho ...
  • maisha ya kiucha-Mungu ni maisha ya aina gani? Je misngi ya maisha hayo haipingani na misingi mikuu ya maisha yetu?
    13570 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Iwapo sisi tutailelekea Qur-ani Tukufu, kisha tukaiuliza Qur-ani swali lifualato: je sisi tumeumbwa kwa ajili gani? Hapa tutaiona Qur-ani ikitujibu kwa kauli ifuatayo: " وَ ما خَلَقْتُ الْجِنَّ وَ الْإِنْسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ. " Maana yake ni kwamba: (Mimi (Mola) sikumuumba mwanaadamu wa jini, ila ...
  • Timsahın saxlanılması və digər ölkələrə satışına icazə varmı?
    8290 Sheria na hukumu 2014/05/22
    Təqlid olunan müctehidlərin cavabları bunlardır: Həzrət ayətullah Xamnei (Allah qorusun) Əti haram olan heyvanların saxlanılması və onun hətta, bu heyvanların ətlərinin yeyilməsini halal bilənlərə də satılması düzgün deyildir. Amma, aqillər nəzərində halal mənfəətə görə olsa məsələn, ətinin başqa ət yeyən heyvanlar üçün istifadəsi yaxud, dərisinin dəri sənətində ...

YALIYOSOMWA ZAIDI