advanced Search
KAGUA
10876
Tarehe ya kuingizwa: 2012/05/06
Summary Maswali
nini hukumu ya kupiga sindano ya nguvu au kutia maji ya nguvu (Intravenous injection) mwilini ndani ya Ramadhani?
SWALI
nini hukumu ya kupiga sindano ya nguvu au kutia maji ya lishe (Intravenous injection) mwilini ndani ya mwezi wa Ramadhani? Je kuna ruhusa ya kutumia vitu kama hivyo? Na je vitu hivyo vyaweza kubatilisha saumu? Na kama sindano hizo zitakuwa ni kwa ajili ya dawa je? Pia zaweza kubatilisha saumu?
MUKHTASARI WA JAWABU

Wanazuoni wamekhitalifiana kuhusiana na suala hilo. Kwa kupata jawabu tosha, ni lazima utuambie kuwa wewe ni mfuasi wa mwanazuoni gani? Ili tuweze kukupa jawabu makini zaidi. Kwa vyovyote vile mitazamo ya baadhi ya wanazuoni wetu ni kama iuatavyo:

Bahjat (r.a) na Khameneiy (Mungu amuhifadhi), wanasema: iwapo sindano hizo zitakuwa ni kwa ajili ya lishe au zitakuwa na aina fulani ya lishe, basi ni bora kua na tahadhari nazo na kujiepusha nazo, lakini zitapokuwa ni kwa ajili ya dawa au kwa ajili ya ganzi, basi hakutokuwa na tatizo kuzitumi sindano hizo.

Fadhil Lankarani (r.a) naye anasema: mwenye saumu anatakiwa kujiepusha na sindano na maji ya kutia nguvu mwilini, lakini hakuna tatizo kupiga sindano za dawa au za ganzi katika hali ya saumu.

Makari Shirazi (Mola amhifadhi) naye anasema: kwa kuchukua hadhari ya kutoharibika funga, ni lazima mtu ajiepushe na sindano za kutia nguvu pamoja na za dawa, pia asitumie maji ya lishe ambayo yanaingizwa kwa mirija maalumu mwilini, lakini hakuna tatizo kutumia sindano za ganzi.

Mwana chuoni Jawadi Tabrizi, Safi Gulpeigani, Nuru Hamadani, Wahidi Kurasani pamoja Sistani wanasema: sindao yeyote ile haiwezi kubatilisha saumu, ewe ni ya kutia nguvu na lishe  au ni kwa ajili ya dawa.[1]

Jawabu kutoka kwa mwanazuoni Ayatullahi Mahdi Hadawiy Tehraniy (Mungu amuhifadhi) ni kama ifuatavyo:

Piga sindano za nguvu (lishe) pamoja na kutia maji ya lishe au ya nguvu mwilini, ni vitu vilivyoko nje ya hukumu ya kula na ya kunywa, ingawaje ni vizuri mtu kujiepusha na aina hiyo ya sindano pamoja na maji ya nguvu au ya lishe.

Kwa ajili ya kupata faida zaidi rejeo zifuatazo ndani ya tovuti hii:

1- funga na utumija wa dawa, swali la 2986 (tovuti: 3479).

2- kutumia spray katika hali ya saumu, swali la 5845 ( tovuti 6063).

 


[1] Taudhihul-Masail Maraaji, ju/1 uk/892 suala la 1576. Ajwibatul- Istiftaat cha Ayatullahi Khameneiy swali la 767. Taudhihul-Masail cha Ayatullahi wahid Khurasaniy, suala la4851.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • ni kwa nini maombolezo ya Imamu Husein (a.s), yakapewa jina la Raudha?
    11466 تاريخ کلام 2012/05/23
    Neno (Raudha) ni neno maalumu linalotumiwa na waombolezaji wa mwauwaji ya Imamu Husein (a.s), na neno hili linatoka kwenye kitabu maarufu cha maombolezo ya Imamu Husein (a.s), kijulikanacho kwa jina la (Raudhatush-Shuhadaa), na kitabu hichi ni moja kati ya vitabu vya mwanzo vilivyonukuu tokeo la Karbala, na ...
  • nini maana ya ucha Mungu?
    21455 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Taqwa (ucha Mungu) ni nguvu maalumu za kiroho zinazo weza kupatikana ndani ya nafsi ya mwanaadamu, nguvu ambazo huwa ni himaya maalumu inayomuwezesha yeye kujitenga na maasi. Taqwa kamili ni ile inayomfanya mtu kujiepusha na maasi yanayo eleweka na kila mmoja wetu, pamoja na kujiepusha na yale ...
  • ni namna gani Qur-ani imelielezea fungamno juu ya imani na kupatikana kwa utulivvu wa moyo?
    12533 Tafsiri 2012/06/17
    Kilugha panapotumika neno Imani au itikadi, humaanisha kule mtu kukubali na kusadiki, na maana hii huwa ni kinyume cha neno kukadhibisha na kukanusha. Kitaalamu neno imani huwa linamaanisha kule mtu kusadiki na kuamini jambo fulani kimatamshi, kimoyo pamoja na kimatendo, lakini neno utulivu ambalo ni tafsiri ya ...
  • je majina ya watu watano watukufu yametajwa ndani ya Taurati na Injili?
    12829 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Kwa mujibu wa nukuu za baadhi ya Hadithi ni kwamba, majina ya matano ya Aali Abaa (a.s), yaani Aali wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambao ni: Ali, Fatima,Hasan na Husein, yametajwa ndani ya Taurati na Injili. Pia suala hilo linaonekana kuashiriwa ndani ya ile Hadithi yenye kunukuu majadilianao ...
  • je nini wajibu wa mwanamke anayenyonyesha kwa muda wa miaka miwili mfululizo? Hivi yeye atatakiwa kulipa fidia ya funga zake pamoja na kuzilipia fidia kwa kutokana na kuchelewesha kuzilipa funga hizo?
    11663 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Jawabu kutoka ofisi ya Ayatullahil-Udhmaa Sistani (Mola amlinde): 1-mwanamke ambaye ananyonyesha, aliye na uchache wa maziwa, awe ni mama wa mtoto au mlezi anayelipwa kwa ajili ya kumnyonyesha mtoto huyo, au hata kama atakuwa anamnyonyesha bure, iwapo funga itakuwa ni yenye kumletea madhara au kumletea ...
  • Shin aure yana da wasu sharaDai na musamman?.
    7053 Sheria na hukumu 2017/05/22
    A mahangar musulunci auren da’imi da na mutu’a suna da sharaDai waDanda sune kamar haka:- 1. Karanto siga (Yarjewa juna tsakanin miji da mata shi kaDai bai wadatar ba lalle ne a hada shi da furta “farar da” lafazi na musamman). 2. Bisa ihtiyaDi na wajibi ya ...
  • nini maana ya itikafu
    20533 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • nini siri hasa ya Uslamu kuwa ni dini ya mwisho, na nini pingamizi hasa ya bwana Surush juu ya hilo?
    14621 Elimu ya zamani ya Akida 2014/02/12
    Kuzingatia nukta zifuatazo kutaweza kumsaidia msomaji kulitambua vyema suala hili: 1- Hitimisho la utume lina maana ya hitimisho la dini; na hii inamaanisha kuwa hakutokuja mtume mwengine baada Yake (s.a.w.w). Hayo pia utayakuta kwenye Aya ya 40 ya Suratul-Ahzab. 2- Dini ya Kiislamu imeitwa dini ya mwisho ...
  • maisha ya kiucha-Mungu ni maisha ya aina gani? Je misngi ya maisha hayo haipingani na misingi mikuu ya maisha yetu?
    13570 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Iwapo sisi tutailelekea Qur-ani Tukufu, kisha tukaiuliza Qur-ani swali lifualato: je sisi tumeumbwa kwa ajili gani? Hapa tutaiona Qur-ani ikitujibu kwa kauli ifuatayo: " وَ ما خَلَقْتُ الْجِنَّ وَ الْإِنْسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ. " Maana yake ni kwamba: (Mimi (Mola) sikumuumba mwanaadamu wa jini, ila ...
  • Timsahın saxlanılması və digər ölkələrə satışına icazə varmı?
    8290 Sheria na hukumu 2014/05/22
    Təqlid olunan müctehidlərin cavabları bunlardır: Həzrət ayətullah Xamnei (Allah qorusun) Əti haram olan heyvanların saxlanılması və onun hətta, bu heyvanların ətlərinin yeyilməsini halal bilənlərə də satılması düzgün deyildir. Amma, aqillər nəzərində halal mənfəətə görə olsa məsələn, ətinin başqa ət yeyən heyvanlar üçün istifadəsi yaxud, dərisinin dəri sənətində ...

YALIYOSOMWA ZAIDI